Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi akiyafunguwa Mafunzo ya siku Tatu ya Uongozi
kwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania bara hapo
Hoteli ya White Sand nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Kushoto ya
Balozi Seif ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambae ndie mwenyeji wa
Mafunzo hayo Mh. Sadiq Meki Sadiq.
Baadhi ya Wakuu wa Mikoa ya Tanzania
Bara wanaohudhuria mafunzo ya Uongozi wakifuatuilia Hotuba ya Mgeni
rasmi wa ufunguzi wa mafunzo hayo Balozi Seif hayupo pichani.
Balozi Seif akiwa katika picha ya
pamoja na Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara
wanaohudhuria mafunzo ya siku tatu ya Uongozi yanayofanyika Hoteli ya
White Sand Mjini Dar es Salaam.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif akiagwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Sadiq Meki
Sadiq mara baada ya kuyafungua mafunzo ya siku tatu ya uongozi kwa
wakuu wa mikoa ya Tanzania bara. Picha zote na Hassan Issa wa –
OMPR – ZNZ
PRESS RELEASE:-
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Iddi alisema kutokuwepo kwa mfumo mzuri wa
mawasiliano ya muingiliano wa kiutendaji kati ya Wakuu wa Mikoa na
Maafisa Tawala wa Mikoa ndio masuala ya msingi yanayolalamikiwa na
Wananchi ambayo husababisha huduma finyu zisizokidhi vinavyotolewa
katika sekta za Umma.
Alisema hali hiyo husababisha ongezeko
la rushwa, ubabaishaji wa baadhi ya watumishi katika kutoa maamuzi ya
haraka ndio mambo yanayosababisha urasimu na ucheleweshaji wa mambo
mbali mbali ya maendeleo ndani ya Mikoa.
Balozi Seif alisema hayo wakati
akiyafunguwa mafunzo ya siku tatu ya Uongozi kwa Wakuu wa Mikoa na
Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara yanayofanyika katika Hoteli
ya White Sand nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.
Alisema zipo changamoto za mahusiano na
muingiliano wa kiutendaji miongoni mwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu
Tawala wa Mikoa ambazo husababisha baadhi ya Viongozi hao kutoa
maamuzi peke yao na hatimae kuleta dosari katika utendaji wao.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
alieleza kwamba Mahusiano na Muingiliano wa utendaji kazi baina ya
Viongozi wa Kisiasa na watendaji ni muhimu na yanahitajika kwa ajili
ya kuimarisha Utawala bora pamoja na ukuaji wa Maendeleo ya Taifa.
“ Uhusiano nwa Mkuu wa Mkoa na Katibu
Tawala wa Mkoa hauishii kwenye utendaji kazi za kila siku bali hata
kwenye upangaji wa Mipango ya na upimaji wa utendaji kazi wa nusu
mwaka na ule wa mwaka mzima “. Alisema Balozi Seif.
Balozi Seif alisisitiza kwamba pande
hizo mbili wakati wote zinategemeana katika utekelezajiwa ufanisi wa
majukumu katika ngazi za Mkoa jambo linalohitajika kwa kila mmoja
kuwa na imani kwa mwenzake kwa ajili ya kuendeleza uhusiano katika
uwajibikaji.
Alieleza kwamba kinyume cha mategemeano
hayo Mkoa unaohusika na mikwaruzano ya uwajibikaji utakosa muelekeo
na hatma yake kusababisha msuguano.
Aliwanasihi Wakuu na Makatibu hao
Tawala wa Mikoa kuitumia vyema fursa waliyoipata ili kubadilishana
uzoefu na kujenga mtandao wa mawasiliano na mahusiano kwa ajili ya
kupashana habari na kushauriana.
Aliwataka washiri hao wa mafunzo ya
Mawasiliano ya muingiliano kujenga mshikamano wa maelewano
utakaorahisisha utendaji na kuepuka migogoro isiyo ya lazima.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
aliishauri Taasisi ya Uongozi kuona namna ya kuwahusisha Wakuu wa
Wilaya na Makatibu Tawala wa Wilaya pamoja na viongozi wa Serikali za
Mitaa katika mafunzo kama hayo ili kuwajengea uwezo wa uwajibikaji.
Balozi SDeif alieleza kwamba Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar itakuwa tayari kutoa ushirikiano ili kuona
mpango huo unafanikiwa na kuiwajengea nguvu za utoaji huduma kwa
wananchi watendaji hao wa Serikali.
Alizishauri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa { TAMISEMI } pamoja na Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Idara Maalum ya SMZ kushirikiana katika
kulitekeleza suala hilo.
“ Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kwa
kushirikiana na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum TAMIM
zione namna ya kuwajumuisha watendaji hao katika kuhudhuria mafunzo
yenye kuboredha uongozi katika maeneo yao “. Alisema Balozi Seif.
Mapema Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya
Uongozi Tanzania Profesa Joseph Semboja alisema mafunzo hayo ya siku
tatu kwa Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara
yataendeshwa kwa njia ya majadiliano.
Profesa Semboja Washiriki hao watapa
fursa ya kubadilisha uzoefu pamoja na kutafuta mbinu za kuzitatua
changamoto zinazoikabili Mikoa mbali mbali Nchini Tanzania.
Akimkaribisha Mgeni rasmi kuyafungua
mafunzo hayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa { TAMISEMI } Mh. Hawa Ghasia alisema jumla ya Wakuu
wa Mikoa 20 na Makatibu Tawala wa Mikoa 22 wanahudhuria mafunzo hayo.
Mh. Ghasia alisema Wakuu na Makatibu
Tawala wa Mikoa watakaokosa mafunzo hayo wanatarajiwa kuungana na
Wakuu wa Mikoa na Maafisa Tawala wa Mikoa ya Zanzibar katika mafunzo
yatakayotolewa hapo baadaye Zanzibar.
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar
21/7/2014.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni