Kiongozi wa Boko Haram Abubakar Shekau
Jeshi la Nigeria limesema
limesambaratisha shambulio lililopangwa na wapiganaji wa Boko Haram
katika kijiji cha Bama kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Waasi hao walivamia mji huo hapo
jana asubuhi maafisa wa Nigeria wamesema.
Vyanzo vya usalama vimenukuliwa
vikisema makumi ya wapiganaji wameuwawa, hata hivyo taarifa hizi
hazijathibitishwa.
Kundi la Boko Haram hivi karibuni
limetangaza kuanzisha Dola ya Kiislam katika miji na vijiji ambavyo
wanavishikilia kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni