Mke wa rais wa zamani wa Afrika
Kusini, Bi. Graca Machel, amesema Uganda inapaswa kuwa na rais mwanamke,
pindi Rais Yoweri Museveni atakapong'atuka.
Bi. Graca ambaye ni mwanaharakati wa
kimataifa wa haki za wanawake na watoto amesema Uganda ni moja ya
nchi za Afrika zenye wanawake wenye akili ambao wanauwezo wa kuwa
rais.
Hata hivyo Bi. Graca alionyeshwa
kusikitishwa baada ya kutaarifiwa kuwa Dk. Specioza Wandira Kazibwe
hayupo tena katika nafasi ya makamu wa rais wa Uganda.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni