Chama cha Taifa cha Wauguzi nchini
Kenya kimesitisha mgomo wake uliopangwa kuanza kesho.
Hatua hiyo inafuatia amri
iliyotolewa na mahakama ya kazi, kutaka mgomo huo usitishwe kufuatia
kesi iliyofunguliwa na mwanaharakati Okiya Omtata, kuupinga.
Jaji Nzioko wa Makau ametoa mari ya
kusitishwa mgomo huo hadi hapo kesi hiyo ya kupinga mgomo wa wauguzi
Kenya, itakaposikilizwa Desemba 11.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni