Mtandao huu umeshuhudia msururu mkubwa wa magari yanayokwenda mikoa ya njombe Ruvuma Mbeya na nchi jirani, pamoja na yanayotoka kwenye mikoa hiyo kwenda Iringa Dodoma, Dare es Salaam na mikoa mingine yakiwa yamekwama kwenye msururu huo.
Ajali hiyo imetokea eneo la Nyororo mkoani Iringa. Baadhi ya abiria na madereva wa malori waliokuwa eneo la tukio wamelalamikia ufinyu vya kulitoa lori hilo kuwa ni hafifu hali iliyopelekea wakae hapo muda mrefu(karibia siku moja).
Hali hiyo iliondolewa majira ya saa tatu asubuhi baada ya lori hilo kufanikiwa kuondolewa barabarani na kusogezwa pembeni ndipo magari hayo yakaendelea na safari. ( Kwa hisani ya Edwin Moshi wa Eddy Blog)
Tayari barabara imefunga, magari hayawezi kupita foleni ni kubwa
Barabara imefunga pande zote mbili hakuna pa kupita
Msusuru wa magari kama unavyoonekana kufuatia ajali hiyo
Jitihada za kulitoa.













Hakuna maoni :
Chapisha Maoni