Ruto na Mkewe Rachel akikata keki
jana kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake katika viwanja vya kanisa.
Naibu rais wa Kenya William Ruto
amewashauri viongozi wa upinzani kuachana na mpango wa kuitisha
maandamano makubwa kupinga Sheria ya Usalama iliyofanyiwa mabadiliko
2014.
Bw. Ruto amesema maandamano hayawezi
kutumika kama ndio njia pekee mbadala ya kutatatua matatizo
yanayoikabili Kenya.
Akiongea kwenye ibada jana kwenye
kanisa la AIC Ziwa katika kaunti ya Uasin-Gishu Bw. Ruto amewataka
viongozi kutumia njia za Kidemokrasia kutoa maoni yao badala ya
kutumia nguvu ya umma.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni