Vikosi vya Wakurdi vimefanikiwa
kuwatimua wapiganaji wa Dola ya Kiislam (IS) katika mji wa Kobane, na
kumaliza mapigano yaliyodumu kwa muda wa miezi minne, katika mji wa
Syria.
Wapiganaji wa Kikosi cha Kujilinda cha
Wakurdi, wamesema wameingia katika eneo la Mashariki la mji wa
Kobane, baada ya wapiganaji wa kundi la IS kuzidiwa nguvu na
kuondoka.
Mji Kobane unaonekana kuwa ni moja ya
mtihani mkubwa wa kimkakati kukabiliana na IS katika nchi ya Syria
kwa kutumia mashambulizi ya anga.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni