.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 29 Januari 2015

WAZIRI MKUU ASEMA SERIKALI ITAKUWA TAYARI KUONGEZA MUDA ZOEZI LA BVR

Serikali imesema kuwa ipo tayari, kuongeza muda wa kuandikisha watu katika daftari la kudumu la wapigakura kwa mfumo wa kielektroniki wa BVR, iwapo Tume ya Uchaguzi (NEC) itakabiliana na matatizo wakati wa uandikishaji na kuiomba serikali kufanya hivyo.

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda ametoa kauli hiyo leo wakati akijibu swali la kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, Mhe. Freeman Mbowe aliyehoji, uwezo wa kuandikisha wapigakura milioni 24, kwa muda uliowekwa wakati mashine za BVR zinauwezo wa kuandikisha watu 22 tu kwa siku.

Mhe. Pinda amesema taarifa alizonazo kutoka kwa Tume ya Uchaguzi ni kuwa awali mashine hizo zilikuwa na uwezo wa kuandikisha watu 74 kwa siku, lakini baada ya kufanyiwa majaribio tume ya uchaguzi ilibaini kuwa zinauwezo wa kuandikisha mara mbili ya idadi hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni