Waziri Mkuu wa Japan ameshutumu video
yenye kitendo kisicho kubalika na chenye kuchochea ghadhabu cha
kuuwawa kwa raia wake Haruna Yukawa na kundi la dola ya Kiislam (IS).
Wazhiri Mkuu huyo Bw. Shinzo Abe
ametaka kuachiwa kwa mateka mwingine Kenji Goto, aliyeonyeshwa kwenye
video hiyo. Japan imesema inajaribu kuthibitisha picha za video hiyo.
Siku ya jumanne, kundi la (IS) lilisema
litawauwa wajapan wawili hao inaowashikilia iwapo hawajalipwa dola
milioni 200 na Japan ndani ya saa 72.
Kenji Goto raia wa Japan anayeshikiliwa na kundi la IS
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni