Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe
amefunguliwa mashtaka ya kuwafukuza kimakosa maafisa wawili
waandamizi wa chama tawala cha Zanu-PF.
Viongozi hao wawili walifukuzwa
kwenye chama hicho mwezi Desemba na Februari kwa madai ya kuunga
mkono jitihada za kumg'oa madarakani rais Mugabe.
Maafisa hao Ruagare Gumbo na Didymus
Mutasa wamewasilisha nyaraka za kesi zao kwenye Mahakama Kuu ya
Zimbabwe wakiitaka itoe amri ya kurejeshewa madaraka yao katika chama
cha Zanu-PF.
Bw. Gumbo ameviambia vyombo vya
habari kuwa rais Mugabe ni dikteta ambaye anapaswa kuachia madaraka.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni