Kocha Luis Enrique amekataa kukanusha
iwapo Barcelona na Manchester United wamekuwa katika mazungumzo
kuhusiana na mchezaji Neymar.
Bosi huyo wa klabu ya Catalan
amekataa kugusia habari zilizoibuka mwishoni mwa wiki kuwa kocha
Louis van Gaal anataka kumnasa mshambuliaji huyo raia wa Brazil.
Aidha, Ed Woodward alionekana
Barcelona wiki iliyopita na kuibua uvumi Manchester United inajaribu
kulazimisha uhamisho huo kabla ya kufungwa kwa kipindi cha uhamisho.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni