Kocha Rafa Benitez ameanza kibarua
cha kuinoa Real Madrid kwa kutofanya vyema katika La Liga baada ya
timu yake kulazimishwa sare tasa na timu iliyopanda daraja ya
Sporting Gijon.
Real Madrid ikiwa imefunga magoli 11
katika michezo nane ya kujiandaa na msimu, imejikuta ikiachia pointi
mbili muhimuna kuwa nyuma ya Barcelona na Atletico Madrid baada ya
kumalizika kwa raundi ya kwanza ya mechi za La Liga.
Mchezo huo ulikuwa wa kwanza kwa
kocha Banitez nchini Hispania tangu miaka 11 kupita alipoondoka
Valencia kwenda Uingereza kuinoa Liverpool.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni