Aliyewahikuwa Waziri wa Mambo ya
Ndani wa Tanzania Laurence Masha, leo amefikishwa katika Mahakama ya
Hakimu Mkazi Jijini Dar es Salaam na kusomewa shtaka.
Akiwa mbele ya Hakimu Waliyarwande
Lema, Masha amesomewa shtaka la kutoa lugha ya matusi kwa Afande Juma
Mashaka jana jioni katika kituo cha polisi cha Oysterbay Jijini Dar
es Salaam alipoenda kuwawekea dhamana vijana 17 wa kundi maarufu la
linalojulikana kwa jina la Kingereza kama 4U Movement.
Mshtakiwa Masha alikana shtaka hilo,
na kupewa sharti la dhamana ya shilingi milioni 1 pamoja na wadhamini
wawili, lakini alishindwa kutimiza masharti ya dhamana kutokana na
muda wakazi kuishi na kurejeshwa rumande, kesi yake itasikilizwa tena
tarehe 7 mwezi ujao.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni