Watu wanne wanaosadikiwa kuwa ni
Majambazi wameuwawa katika majibishano Makali ya risasi na Jeshi la
Polisi katika eneo la Chapwa lililopo nje kidogo ya mji wa Tunduma
Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya.
Tukio hilo limetokea wakati
Majambazi hao walipo jaribu kumteka wakala wa kampuni ya TBL Thadeo
Sanga na kumpora kiasi cha shilingi laki mbili ,gari aina ya Suzuki
V6 T215 BLZ Pamoja na Bastola yake yenye numba 815859.
Wakizungumza na kituo hiki wameeleza
kuwa baada ya uporaji huo majambazi hao walifanikiwa kutoweka eneo la
tukio kwa kutumia gari la wakala huyo ambalo hata hivyo baadaye
liliwashinda na Kupinduka.
Aidha wakiwa katika hali ya
sintofahamu majambazi hao walitelekeza gari na kukimbilia porini ili
kujiokoa huku wakifwatiliwa na wananchi kwa kushirikiana na Jeshi la
Polisi.
Majambazi hao ambao hata hivyo
hawakutambulika majina na Makazi waliko toka walikutwa na Bunduki
mbilia aina ya SMG na Steering Gun ambazo zilikuwa zinatumiwa na
majambazi hao kwa uporaji.
Miili ya marehemu hao ambao
wameuwawa kwa ujmbazi imehifadhiwa katika Hospitali ya wilaya ya
Momba ikisubili utambuzi wa ndugu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni