Timu ya Arsenal imepata ushindi wa
mabao 2-1 dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya Uingereza timu ya Leicester
City katika mchezo ambao wageni Foxes walimaliza wakiwa na wachezaji
10 katika dimba la Emirates.
Leicester City walipata bao lao
kupitia kwa mshambuliaji wao nyota Jamie Vardy ambaye alipewa penati
yenye utata na yeye kutofanya ajizi na kuutumbukiza kimiani mpira huo
wa adhabu.
Danny Simpson alilambwa kadi
nyekundu baada ya kuwa tayari na kadi ya njano ya kwanza kwa kucheza
rafu, huku Theo Walcott aliyetokea benchi akiisawazishia Arsenal
zikiwa zimebakia dakika 20 mpira kuisha naye Danny Welbeck aliyerejea
uwanjani akitokea kwenye majeruhi akifunga mpira wa kichwa dakika za
nyongeza na kuipa Arsenal ushindi.
Jamie Vardy akishangilia goli la penati na wachezaji wenzake wa Leicester City
Danny Simpson akishika kichwa asiamini kadi nyekundu aliyopewa
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni