.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 12 Februari 2016

MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA UHALIFU YA (ICC) KUTOA UAMUZI WA RUFAA YA RUTO

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ya (ICC) leo itatoa uamuzi wa rufaa iliyofunguliwa na Naibu Rais wa Kenya, William Ruto, rufaa ambayo itatoa msimamo wa kesi inayomkabili katika mahakama hiyo.

Majaji wa rufaa wa mahakama hiyo ya ICC, wataamua kama ushahidi uliorekodiwa siku za nyuma usiwasilishwe katika kesi inayowakabili Ruto na mwandishi wa habari Joshua Sang.

Rekodi zinaonyesha kwanini mwendesha mashtaka Fatou Bensouda, anataka ushahidi huo ubakie mahakamani, na kwanini mawakili wa washtakiwa wanataka ushahidi huo uliorekodiwa kuondolewa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni