Bunge la Afrika Kusini jana
lilitibuka kwa muda baada ya kugeuka uwanja wa ngumi kwa wabunge
kutupiana makonde, baada ya vyombo vya dola kuamuriwa kuwatoa wabunge
wa upinzani walioleta fujo wakati rais Jacob Zuma akihutubia bunge.
Wabunge hao wa chama cha mrengo wa
kushoto cha Economic Freedom Fighters (EFF), walionekana kukerwa na
amri hiyo na kuanza kupambana na wenzao wakati walipotolewa kwa nguvu
bungeni kwa kumzomea rais Zuma.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni