.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 24 Machi 2017

LIONEL MESSI AIBEBA ARGENTINA KUWANIA KUFUZU KOMBE LA DUNIA

Kapteni wa Argentina Lionel Messi ameifungia nchi yake goli katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Chile huko Buenos Aires na kuimarisha matumaini ya Argentina kufuzu michuano ya Kombe la Dunia.

Mchezaji wa Chile Jose Pedro Fuenzalida alimuangusha Angel Di Maria kwa kumsukuma kwa nyuma na kusababisha kutolewa penati.

Mfungaji nyota wa Argentina Lionel Messi aliipiga penati hiyo kwa utulivu iliyompita kipa Claudio Bravo ikiwa ni siku 269 kupita tangu akose penati dhidi ya Chile katika finali ya Copa Amerika.
             Angel Di Maria akilalamika kwa refa baada ya kusukumwa chini na Jose Pedro
                            Lionel Messi akiwa amempoteza mahesabu kipa Claudio Bravo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni