Arsenal imekosa nafasi ya kutinga
Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka
20, licha ya kuifunga Everton kwa magoli 3-1.
Kikosi cha kocha Arsene Wenger
kilipata ushindi wanaostahili licha ya beki Laurent Koscielny
kutolewa nje kwa kucheza rafu ya kizembe.
Arsenal walipata goli lao la kwanza
kupitia kwa Hector Bellerin na kisha kuongeza la pili kupitia kwa
Alexis Sanchez na latatu la Ramsey. Romelu Lukaku alifunga kwa
penati.
Kocha Arsene Wenger akiwa ameinamisha kichwa chini baada ya kuikosa nafasi ya nne Ligi Kuu ya Uingereza
Hata hivyo Liverpool ilihakikisha
haikosi nafasi ya nne baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi
ya Middlesbrough na kufanikiwa kushiriki Ligi ya Mabingwa.
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp akishangilia kufanikiwa kumaliza katika nafasi ya nne Ligi Kuu ya Uingereza
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni