Arsenal inahakikisha mbio za kuwania
kumaliza katika nafasi ya nne katika Ligi Kuu Uingereza zinaamuliwa
hadi dakika ya mwisho baada ya kupata ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya
Sunderland.
Katika mchezo huo wa jana Alexis
Sanchez alifunga goli la kwanza akiunganisha pasi ya Mesut Ozil
katika dakika ya 72 na kuamsha hamasa katika dimba la Emirates.
Goli hilo liliamsha hamasa kwa
Arsenal na kulishambulia goli la Sunderland na alikuwa Sanchez
tena aliyefunga goli la pili akinasa mpira uliopigwa na Olivier
Giroud.
Alexis
Sanchez akifunga goli lake la kwanza katika mchezo huo
Alexis
Sanchez akitumbukiza goli la pili akinasa mpira uliopigwa na Giroud
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni