Kipa Sergio Romero ameokoa kiufundi
michomo kadhaa wakati Southampton na Manchester United wakitoka sare
katika dimba la St Mary's.
Southampton walikuwa waongoze katika
dakika ya tano wakati Eric Bailly kumkamata mchezaji katika eneo la
penati, lakini kipa United, Romero akaokoa penati ya Manolo
Gabbiadini.
Shoti kali la Bailly nalo
liliokolewa na kipa Fraser Forster, baada ya beki huyo kutengeneza
nafasi nzuri katika kipindi cha kwanza cha mchezo.
Southampton walimpa kazi ya ziada
kipa Romero ya kuokoa mashuti yao, huku naye Anthony Martial akiachia
shuti la umbali wa yadi 25 lililogonga mwamba.
Manolo
Gabbiadini akipiga mpira wa penati huku wachezaji wenzake wakiufuatilia kwa kuuangalia
Kipa wa Manchester United Sergio Romero akiufuata mpira wa penati uliopigwa na kuupangua
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni