.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 28 Mei 2017

MESSI AISAIDIA BARCELONA KUTWAA KOMBE LA COPA DEL REY

Lionel Messi ameisaidia Barcelona kuifunga Alaves magoli 3-1 na kutwaa ubingwa wa kombe la Copa del Rey kwa mara ya tatu mfululizo.

Ushindi huo ni zawadi kwa kocha wao Luis Enrique ambaye anaacha kuinoa klabu hiyo baada ya kuwa nayo kwa miaka mitatu.

Mchezaji Ibai Gomez aliachia shuti lililogonga mwamba wa goli la Barcelona kabla ya baadaye Messi kufunga goli lake la 54 katika msimu huu kwa shuti la mpira wa kuzungusha.

Hata hivyo Theo Hernandez alifunga kwa mpira wa adhabu na kusawazisha goli hilo, lakini Mbrazil Neymar alifunga goli la pili na Paco Alcacer akigongeana na Messi akatupia la tatu.
   Wachezaji wa Barcelona wakiwa katika picha ya pamoja na kombe lao la Copa del Rey
                         Kocha Luis Enrique akiwa amenyanyua juu kombela Copa del Rey

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni