Msichana wa miaka 23 nchini India
amemkata sehemu za siri kiongozi wa kiroho wa Kihindu katika jimbo
la kusini la Kerala, kwa madai kuwa alikuwa akimbaka kwa miaka mingi.
Polisi wamesema mtuhumiwa
anayejulikana kwa jina la Gangeshananda Theerthapada, alikuwa akienda
kwenye nyumba ya msichana huyo kufanya matambiko kwa ajili ya afya ya
baba yake.
Mama wa msichana huyo alikuwa na
matumaini kuwa kiongozi huyo wa kiroho atasaidia kutakasa mikosi
inayoiandama familia yake, lakini sasa mtoto wake amedai alikuwa
akimbaka kila mara.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni