Nyota wa Manchester United, Paul
Pogba, amekwea pipa na kutua nchini Saudi Arabia na kushiriki siku ya
kwanza ya mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani ikiwa ni siku tatu tu
kupita tangu abebe kombe la Ligi ya Uropa.
Pogba aliyevalia vazi la kitambaa
cheupe akiwa amekata nywele zake kwa mtindo mpya wa nywele fupi
alionekana miongoni mwa mahujaji waliokuwa katika mji wa Makka baada
ya kuanza mfungu wa Ramadhani siku ya jumamosi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka
24, ambaye ni muumini wa dini ya Kiislamu, haijajulikana iwapo
atafunga mwezi mzima wa Ramadhani, huku akiwa ameitwa katika kikosi
cha kocha Didier Deschamp wakati Ufaransa itakapowavaa Paraguay,
Sweden na Uingereza mwezi Juni.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni