Mwanafamilia wa familia ya kifalme
ya Japan, Princess Mako, ataachia hadhi ya ufalme, kutokana na kuamua
koolewa na mwanaume anayetoka kwenye koo isiyo ya kifalme.
Princess Mako, 25, ambaye ni mjukuu
wa Mfalme Akihito ataolewa na mfanyakazi wa kampuni ya sheria aitwaye
Kei Komuro mwenye miaka 25 pia ambaye alikutana naye masomoni.
Japan inasheria kali zinazomtaka
mwanafamilia wa kifalme wa kike kuondoka katika familia ya Kifalme
baada ya kuolewa na mwanaume kutoka kwenye familia isiyo ya kifalme.
Kei Komuro mwanaume anayemuoa Princess Mako
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni