Cristiano Ronaldo amevunja rekodi
aliyoweka Jimmy Greaves miaka 46 ya rekodi ya kufunga Ulaya wakati
Real Madrid ikisogea na kubakisha pointi moja tu kuweza kutwaa
ubingwa wa La Liga tangu mwaka 2012.
Ronaldo aliifungia Real Madrid goli
la kwanza na kufanya kufikia magoli 367 katika ligi tano za juu za
Ulaya, na kufikia rekodi iliyowekwa na mshambuliaji wa zamani wa
Uingereza Greaves mwaka 1971.
Ronaldo akafunga tena goli la pili
baada ya John Guidetti kuipamatumaini Celta iliyokuwa na wachezaji 10
kwa kufunga goli, huku mshambuliaji Mfaransa Karim Benzema na Toni
Kroos wakifunga nao goli moja kila mmoja.
Real Madrid watatangazwa kuwa
mabingwa wa La Liga jumamosi iwapo watatoa sare tu na Malaga ambayo
ipo katika nafasi za kati katika msimamo wa ligi.
Cristiano Ronaldo akijipinda na kuachia shuti lililozaa goli
Mpira uliopigwa na Cristiano Ronaldo ukiwa umejaa wavuni
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni