Timu ya Monaco imeshinda Ubingwa wa
Ligi 1 kwa mara ya kwanza tangu miaka 17 kupita, baada ya jana
kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Saint-Etienne.
Ikiwa inahitaji pointi moja tu
kutawazwa kuwa mabingwa wa ligi hiyo ya Ufaransa kwa mara ya nane,
mchezaji aliyekatika kiwango bora kinda Kylian Mbappe alifunga goli
la kwanza kiufundi.
Mbappe, 18, aliufuata mpira
uliopigwa na kapteni Radamel Falcao na kudokoa juu ya kipa na kisha
kuutumbukiza kimiani.
Mshambuliaji Valere Germain
aliihakikishia ushindi Monaco kwa kufunga goli la pili katika dakika
za mwisho.
Kinda Kylian Mbappe akifanya vitu vyake katika mchezo wa jana
Wachezaji wa Monaco wakifurahia kutwaa kombe la ubingwa wa Ligi 1
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni