Ripoti zinaeleza kuwa watu wengi
wapatao 140, wakiwemo raia wamekufa katika shambulizi kwenye kambi ya
uwanja wa ndege wa jeshi nchini Libya.
Awali ilizaniwa kuwa watu 60
walikufa wakati wapiganaji wanaoungwa mkono na serikali walipokuwa
wakijaribu kutwaa kambi hiyo ya Brak al-Shati siku ya Alhamisi.
Waziri wa Ulinzi wa Libya wa
serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa pamoja na kamanda wa
wapiganaji wote wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi.
Waziri Mkuu wa Libya amekanusha
kutoa amri ya kufanyika kwa shambulizi hilo lililosababisha vifo vya
watu wengi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni