.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 21 Mei 2017

WAZIRI HAMAD AIPIGIA DEBE ZANZIBAR

unnamedWaziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (kushoto) akimkabaribisha Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB), Bw. Francis Assenga (kulia) wakati walipomtembelea Ofisini kwake mjini Unguja.
A
Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Chacha (wapili kushoto) akikaribishwa na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (kulia) wakati viongozi wa TADB walipomtembelea Mhe. Waziri Ofisini kwake mjini Unguja. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (wapili kulia) na Meneja Mikopo wa TADB, Bw. Samuel Mshoto.
A 1
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi Maryam Juma Abdullah (aliyesimama) akizungumza wakati ugeni kutoka TADB ulipomtembelea Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed Ofisini kwake mjini Unguja.
A 3
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (aliyesimama) akieleza dhima ya Benki ya Kilimo wakati walipomtembelea Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (wapili kulia).
A 5
Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (aliyesimama) akizungumza na ugeni kutoka TADB. Katika mkutano huo Mhe. Waziri aligusia fursa lukuki za uwekezaji katika kilimo visiwani Zanzibar.
A 7
Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (aliyesimama katikati) akifafanua kuhusu sursa za za uwekezaji zilizopo Zanzibar wakati wa mkutano wake na ugeni kutoka TADB. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo, Bw. Francis Assenga (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi Maryam Juma Abdullah (kulia).
A 6
Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (aliyesimama) akihimiza kuhusu umuhimu wa TADB kuwekeza Visiwani humo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anaeshughulikia Kilimo na Maliasili Bibi Maryam Juma Abdullah.
A 8
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga (aliyesimama) akitoa ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali juu ya huduma za Benki ya Kilimo kwa Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed (kulia). Kushoto Mkurugenzi wa Mikopo na Biashara wa TADB, Bw. Augustino Chacha.
A 9
Ugeni wa Benki ya Kilimo wakiwa katika ya pamoja na Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar na maafisa wa Wizara hiyo.

Na Mwandishi wetu,

Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Hamad Rashid Mohamed amesema sasa ni wakati muafaka kwa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania (TADB) kuwekeza Visiwani Zanzibar ili kuchagiza juhudi za Serikali za kuwawezesha kiuchumi wakazi wa visiwa hivyo wanaojishughulisha na sekta za kilimo, uvuvi na uchakataji mazao.

Mhe. Hamad amesema Visiwa vya Zanzibar vina maeneo mengi ya uwekezaji yenye kuweza kuongeza tija na ongezeko la uchumi visiwani humo ikiwa kutakuwa na uwekezaji mkubwa katika maeneo hayo.

“Nawahakikishia, mkianza kuwekeza katika miradi kama ya mwani, uvuvi na karafuu Bebki itapata matokeo makubwa sana na mnaweza kuitumia Zanzibar kama mfano rejea katika utoaji wa mikopo yenye tija nchini,” alisihi.

Kwa mujibu wa Mhe. Waziri, Zanzibar ni miongoni mwa visiwa vyenye utajiri mkubwa ambavyo kukiwa na uwekezaji wa kimkakati vinaweza kutokea matokeo makubwa na yenye kuwanufaisha wananchi wengi.

Akizungumza na Mhe. Waziri, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Francis Assenga amesema Serikali iliamua kuanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ili kusaidia kukabiliana na mapungufu ya wakulima nchini kote ili kuhuisha upatikanaji wa mikopo katika sekta ya kilimo na kuchagiza mapinduzi katika kilimo nchini.

Bw. Assenga ameongeza kuwa Benki inatambua fursa za uwekezaji Visiwani Zanzibar na amemuahidi kuwa wamejipanga kuanza uwekezaji mkubwa wa wadau wa sekta za kilimo na uvuvi ambazo ni sekta za kipaumbele zinazopatiwa mikopo na TADB.

Ameongeza kuwa Benki yake imejipanga kuendeleza uongezaji wa thamani wa sekta hizo ili kuongeza tija sekta hizo ili kupambana na umaskini nchini.

TADB ni taasisi ya serikali ambayo ilianzishwa kwa ajili ya kutatua ufinyu mkubwa wa upatikanaji wa fedha mikopo kwa ajili ya maendeleo ya kilimo nchini ambao ulikuwa unachangiwa kwa kiasi kikubwa na mikopo mingi kutoka taasisi za fedha kuelekezwa zaidi kwenye upande wa biashara za bidhaa; riba kubwa kwenye mikopo ya kilimo; mikopo ya muda mfupi; masharti magumu ya kukopa bila kuzingatia hali halisi ya sekta ya kilimo na mazao ambayo inaathiriwa kwa kiasi kikubwa na mabadiliko ya hali ya hewa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni