.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 17 Mei 2017

WAZIRI WA ZAMANI WA INDIA AMALIZA ELIMU YA SEKONDARI AKIWA GEREZANI

Waziri wa zamani wa India anayetumikia adhabu ya kifungo jela kwa rushwa amefaulu mtihani wa kumaliza elimu ya sekondari akiwa na umri wa miaka 82.

Waziri huyo Prakash Chautala, aliyekuwa waziri kwa mihula minne katika jimbo la kaskazini la Haryana, alifanya mtihani wa kidato cha 12 akiwa gereza la Tihar Jijini Delhi.

Mtoto wake Abhay Chautala amesema baba yake ameamua kutumia kuutumia kwa manufaa muda anaotumikia kifungo jela kwa kusoma.

Waziri huyo wa zamani wa Haryana alitiwa hatiani kwa tuhuma za rushwa katika zoezi la kuwaajiri walimu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni