Waziri wa zamani wa India
anayetumikia adhabu ya kifungo jela kwa rushwa amefaulu mtihani wa
kumaliza elimu ya sekondari akiwa na umri wa miaka 82.
Waziri huyo Prakash Chautala,
aliyekuwa waziri kwa mihula minne katika jimbo la kaskazini la
Haryana, alifanya mtihani wa kidato cha 12 akiwa gereza la Tihar Jijini Delhi.
Mtoto wake Abhay Chautala amesema
baba yake ameamua kutumia kuutumia kwa manufaa muda anaotumikia
kifungo jela kwa kusoma.
Waziri huyo wa zamani wa Haryana
alitiwa hatiani kwa tuhuma za rushwa katika zoezi la kuwaajiri
walimu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni