Bingwa mtetezi Novak Djokovic
ametolewa nje katika michuano ya wazi ya Ufaransa, kufuatia kufungwa
seti zote na Dominic Thiem.
Djokovic raia wa Serbian
anayeshikilia nafasi ya pili kwa ubora alijikuta akifungwa na Thiem,
kwa seti 7-6 (7-5) 6-3 6-0 Jijini Paris.
Ushindi huo wa Muastralia Thiem
anayeshikilia nafasi ya namba sita kwa ubora ni wa kwanza dhidi ya
Djokovic na sasa atavaana na Rafael Nadal katika hatua ya nne bora.
Nadal ametinga nusu fainali baada ya
Mhispania mwenzake Pablo Carreno Busta kujitoa katika mchezo wao
kutokana na maumivu ya tumbo wakati matokeo yakiwa 6-2 2-0.
Dominic Thiem akijiandaa kuupiga mpira uliopigwa na Novak Djokovic
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni