Nyota wa Real Madrid, Cristiano
Ronaldo ametetea nafasi yake ya kuwa kinara wa wachezaji wanaolipwa
fedha zaidi kwa mujibu wa takwimu za mwaka za jarida la Forbes lenye
orodha ya wachezaji 100.
Ronaldo, 32, anajiingizia kitita
cha dola milioni 93 kwa mwaka na kumfanya mchezaji huyo raia wa Ureno
kuongoza wachezaji wenzake kwa mwaka wa pili mfululizo, kwa
kujichumia fedha nyingi.
Kabla ya Ronaldo kutwaa nafasi ya
kwanza kwa kuingiza fedha nyingi wanamichezo waliokuwa wakishikilia
nafasi hiyo ni nyota wa tenesi Tiger Woods na bondia Floyd Mayweather
kwa miaka 15 mfululizo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni