Mchezaji anayewaniwa na Manchester
United, Alvaro Morata, anatarajia kujua mustakabali wake baada ya
wiki mbili.
Wakala wa Morata amefanya mazungumzo
na maafisa wa Real Madrid siku ya Ijumaa na kuweka wazi kuwa anataka
mshambuliaji huyo kuchezeshwa michezo mingi.
Morata ,24, ambaye alifunga goli
jumatano wakati Hispania ikiibuka na sare ya magoli 2-2 dhidi
Colombia, amekuwa akikosa namba mara kwa mara katika msimu ulioisha.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni