Mshambuliaji nyota wa Chelsea Diego
Costa ameambiwa na kocha wake Antonio Conte kuwa hayupo tena kwenye
mipango ya klabu hiyo.
Costa mwenye miaka 28 amefunga
magoli 20 kati ya michezo 35 ya Ligi Kuu ya Uingereza na kuisaidia
Chelsea kutwaa ubingwa, sasa anajiandaa kuondoka Stamford Bridge.
Amesema kuwa Antonio Conte amemtumia
ujumbe unaosema Chelsea haina mpango naye na kuongeza kuwa hamtarajii
kuwapo katika kikosi chake cha msimu ujao.
Costa mzaliwa wa Brazil aliyechukua
uraia wa Hispania amesema uhusiano wake na kocha Conte umekuwa mbaya
katika msimu huu.
Uhusiano baina ya kocha Antonio Conte na Diego Costa haukuwa mzuri msimu huu
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni