Wanaume wenye vipara nchini Msumbiji
wanakabiliwa na mashambulizi ya kutoa kafara, polisi nchini humo
wametahadharisha, kufuatia vifo vya wanaume watatu vipara
vilivyotokea hivi karibuni.
Watuhumiwa wawili wamekamatwa katika
kijiji cha kati cha nchi hiyo cha Milange, ambapo mauaji ya wanaume
wenye vipara yametokea.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Zambezia Afonso Diasa amesema wauaji wanaamini kuwa vichwa vya
wanaume wenye vipara vinadhahabu.
Watu wenye ulemavu wa ngozi nao
wamekuwa wakiuwawa katika Mkoa huo kwa imani za kishirikiana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni