Mwanafunzi wa Chuo Kikuu amejiuwa
huko Shauri Moyo, Jijini Nairobi baada ya kupita wiki mbili tangu
arudishwe nyumbani kwa kukosa ada.
Mwanafunzi huyo Fredrick Kinyanjui,
22, ambaye alikuwa mwaka wa pili katika chuo cha Multimedia,
alikutwa akiwa kajinyonga kwenye paa la nyumba yao jana jioni.
Mkuu wa polisi wa kituo cha Buruburu
DCI Jeremiah Ikiao wachunguzi wamebaini mwanafunzi huyo alirudishwa
nyumbani siku 14 zilizopita kwa kukosa ada.
DCI Ikiao amesema mama wa Kinyanjui
alikuwa ameenda kazini wakati mwanafunzi huyo alipochukua uamuzi wa
kujinyonga.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni