Manchester United inatarajiwa
kutotoa mkataba mpya kwa mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic wakati
mkataba wa hivi sasa utakapoisha Juni 30.
Mwaka jana mchezaji huyo mwenye umri
wa miaka 35, alikubali kuingia mkataba wa mwaka mmoja, ukiwa na
uwezekano wa kuongezwa.
Hata hivyo suala la kuongezewa muda
halijafanyika huku Ibrahimovic akiumia goti mwezi April na kumfanya
kutomaliza msimu.
Timu za Ligi Kuu ya Uingereza
zinatarajiwa kutoa orodha ya wachezaji itakaowabakisha kwa msimu ujao
hii leo.
Zlatan Ibrahimovic akiwa amenyanyua juu kombe la ligi ya Uropa
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni