.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 31 Julai 2017

CRISTIANO RONALDO KUPANDISHWA KIZIMBANI KWA KUKWEPA KODI

Mchezaji Cristiano Ronaldo anatarajiwa kufikishwa Mahakamani nchini Hispania baadaye leo, kwa tuhuma za kukwepa kulipa kodi ya mamilioni.

Waendesha mashtaka wanadai Ronaldo, ambaye inasemekana ni mwanamichezo anayelipwa fedha nyingi duniani, amekwepa kulipa Euro milioni 14.7 sawa na dola milioni 17.3 tangu 2010.

Nyota huyo wa Real Madrid awali alishakanusha tuhuma hizo, na kusema kuwa anachoamini ni kuwa hajawahi kuhusika na kosa lolote la ukwepaji kodi.

Ronaldo, 32, ni miongoni mwa wachezaji wa mpira wa miguu ambao hivi karibuni wamekuwa wakifuatiliwa na mamlaka za kodi za Hispania kwa makosa ya kukwepa kulipa kodi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni