Jon Jones ametwaa tena ubingwa wa
UFC wa uzito wa light heavyweight baada ya kurejea tena ulingoni
tangu kupita mwaka mmoja, kwa kumdunda kwa KO mpinzani wake Daniel
Cormier katika raundi ya tatu.
Pambano lao hilo la marudio baada ya
kupita miaka miwili na nusu tangu wakutane kwa mara ya kwanza,
lilichezwa kwenye ukumbi wa Honda Center, huko Anaheim, baada ya
Jones kuchonga kuwa yeye ni bingwa wa mabingwa katika historia ya
mchezo wa UFC.
Katika raundi mbili za kwanza
mabondia hao walionyesha ushindani wa nguvu na mchezo mzuri
wakipambana bila ya kushikana mara kwa mara, lakini Jones alitumia
vyema teke alilompiga Cormier raundi ya tatu kisha kumshambulia
vilivyo na kumaliza pambano.
Jon Jones akimpiga teke Daniel Cormier lililochangia kumaliza nguvu
Jon Jones akimshindilia ngumi mfululizo Daniel Cormier na kumaliza kabisa
Daniel Cormier akibubujikwa na machozi wakati akihojiwa baada ya kudundwa
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni