Mkurugenzi wa Kitengo cha TEHAMA wa
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC) Chris Musando aliyepotea
Ijumaa usiku amekutwa akiwa ameuwawa, mwili wake ukiwa hauna mkono.
Polisi Kenya wamesema mwili wa
marehemu Musando umekutwa pamoja na mwanamke ambaye bado
hajatambulika katika eneo la Kikuyu na imeshahifadhiwa katika chumba
cha maiti.
Kifo hicho kimetokea ikiwa zimebakia
siku saba tu kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu Agosti 8, mwaka
huu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni