Jose Mourinho amethibitisha kuwa
mchezaji Nemanja Matic anataka mno kujiunga na Manchester United
baada ya kuvuja picha ya mchezaji huyo akifanyiwa vipimo.
Kiungo huyo wa Chelsea atakamilisha
uhamisho wa paundi milioni 40 kuungana tena na Mourinho na inaaminika
picha alionekana Matic kavaa jezi ya United ni ya kweli.
Hata hivyo akiongea baada ya
Manchester United kushinda magoli 3-0 katika mchezo wa kirafiki dhidi
ya Valerenga Jijini Oslo, Mourinho alikataa kuthibitisha kukamilisha
uhamisho wa Matic.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni