Gerard Pique amefunga goli la
ushindi wakati Neymar akisaidia kupatikana kwa magoli mawili katika
mchezo wa El Clasico uliopigwa Marekani ambao Real Madrid ililala kwa
magoli 3-2.
Katika mchezo huo ambao refa
alilazimika kutoa kadi nne za njano, Lionel Messi alikuwa wakanza
kupachika goli wavuni katika dakika tatu tu za mchezo uliochezwa
kwenye dimba la Hard Rock.
Kikosi hicho cha Ernesto Valverde
kiliongeza goli la pili dakika nne baadaye pale Ivan Rakitic
alipounganisha wavuni pasi ya Neymar, kisha baadaye Mateo Kovacic
akachomoa goli moja.
Marco Asensio aliipatia Real Madrid
goli la pili dakika chache baada ya kuanza kipindi cha pili kwa
kuachia shuti lililomshinda kipa Jasper Cillessen, hata hivyo Gerard
Pique aliipatua Barcelona goli la ushindi kupitia krosi ya Neymar.
Lionel Messi akiangalia mpira alioupiga ukienda kujaa wavuni na kuandika goli la kwanza
Mchezaji Ivan Rakitic akifunga goli la pili la Barcelona kwa shuti kali
Marco Asensio akimpiga chenga beki Jordi Alba na kisha kufunga goli la pili la Real Madrid
Gerard Pique akiunganisha krosi ya Neymar na kufunga goli la tatu lililoipa ushindi Barcelona
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni