Kocha Zinedine Zidane ameipa ishara
njema Manchester United kwa kusema kuwa anaweza kushindwa kumbakisha
Gareth Bale, Real Madrid.
Mustakabali wa Bale katika klabu
hiyo yenye maskani yake Bernabeu haujajulikana wakati huo ambapo Real
Madrid ikijipanga kutoa paundi milioni 160 kwa mshambuliaji wa
Monaco, Kylian Mbappe.
Inafahamika kuwa kocha huyo wa Real,
Zidane huenda akalazimika kuwatoa kafara Cristiano Ronaldo, Karim
Benzema ama Bale ili kumpa nafasi Mbappe.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni