Barcelona inatarajia kurejea tena
kwa Liverpool na ofa ya dau la paundi milioni 138 ili kumtwaa
Mbrazili, Philippe Coutinho.
Klabu hiyo kubwa ya Hispania leo
itatoa ofa ya paundi milioni 101 kwanza kwa Liverpool na kisha
baadaye kuongeza kiasi cha paundi milioni 37.
Kiasi hicho cha fedha za nyongeza
kitahusishwa iwapo Coutinho atacheza Ligi ya Mabingwa Ulaya jambo
ambalo litawezekana iwapo akihamia Barcelona.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni