Bondia Wladimir Klitschko ameamua
kustaafu ngumi, na kuuwa matumaini ya kuwepo kwa marejeo ya pambano
lao na Anthony Joshua.
Bondia huyo raia wa Ukraine alipigwa
na Joshua katika pambano la uzito wa juu mwezi Aprili na Muingereza
Joshua alikuwa akitarajia kurejeana naye tena Novemba 11.
Lakini Klitschko mwenye umri wa
miaka 41, ametoa video akithibitisha kuwa ameamua kustaafu rasmi
kupambana ngumu baada ya kuzidunda kwa miaka 21.
Bondia Wladimir Klitschko akipambana na Anthony Joshua
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni