Mshambuliaji Kelechi Iheanacho
amefanyiwa vipimo Leicester City jana kuelekea kukamilisha uhamisho
wa paundi milioni 25 akitokea Manchester City.
Mchezaji huyo raia wa Nigeria,
ameshaafikiana na Leicester kuhusu maslahi yake na sasa anaelekea
kukamilisha kila kitu baada ya saa 24.
Kelechi Iheanacho amekuwa siyo
mchezaji anayepewa kipaumbele katika kikosi cha Manchester City hivyo
kufungua milango ya kuondoka kwake.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni