Mchezaji Daniel Sturriddge ametoka
dimbani kwa maumivu ya paja baada ya kufunga goli wakati Liverpool
ikiifunga Bayern Munich kwa magoli 3-0 katika kombe la Audi.
Mshambuliaji huyo wa Uingereza
alifunga goli dakika 15 baada ya kutokea benchi kwa kufunga goli la
tatu la Liverpool, na kisha kutolewa nje kwa kuumia.
Magoli mengine ya Liverpool
yalifungwa na Msenegali Sadio Mane na Mohamed Salah na kuifanya itinge fainali
dhidi ya Atletico Madrid jumatano.
Mshambuliaji wa Liverpool Sadio Mane akifunga goli
Mshambuliaji mpya wa Liverpool Mohamed Salah akifunga goli kwa mpira wa kichwa
Daniel Sturriddge akigugumia kwa maumivu baada ya kuumia paja
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni