Neymar ameahidi kushinda makombe
mengi wakati akikaribishwa kwa shangwe baada ya kutambulishwa kwa
mashabiki wa Paris St-Germain siku ya jumamosi.
Mshambuliaji huyo raia wa Brazili
amejiunga na klabu hiyo ya Ufaransa akitokea Barcelona kwa ada ya
paundi milioni 200 na atalipwa paundi milioni 40.7 kwa mwaka.
Neymar alilazimika kuangalia PSG
ikishinda 2-0 dhidi ya Amiens kutokana na kutokamilika kwa nyaraka
zake, akishuhudhia Edinson Cavani na Javier Pastore wakifunga magoli.
Neymar akishangilia goli lililofungwa na timu yake mpya ya PSG
Edinson Cavani akiwa amepiga mpira uliomshinda kipa wa Amiens na kujaa wavuni
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni