Mshambuliaji wa Barcelona Neymar
amepewa ruhusa kuanza mazungumzo ya uhamisho wake utakaoweka rekodi
wa kiasi cha paundi milioni 198 kwenda Paris St-Germain.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa
Brazil, amewaambia wachezaji wenzake katika mazoezi hii leo, kwamba
anahitaji kuondoka kwenye klabu hiyo ya Hispania.
Tayari amepewa ruhusa na kocha wa
Barcelona Ernesto Valverde kutoendelea na mazoezi ili aweze
kushughulikia mustakabali wake wa uhamisho.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni