Raheem Sterling ameiokoa Manchester
City iliyobakia na wachezaji 10 na kuinyima Everton ushindi katika
usiku ambao Wayne Rooney alifunga goli lake la 200 la Ligi Kuu ya
Uingereza.
Manchester City walijikuta na
kibarua kigumu baada ya Rooney kufunga goli na baada ya Kyle Walker
kutolewa nje kwa kadi mbili za njano za haraka ndani ya dakika 44.
Kikosi hicho kinachonolewa na Pep
Guardiola hakikuamini matokeo hayo na kilipambana mnono na kufanikiwa
kuepuka kipigo cha pili nyumbani wakiwa chini ya Mhispania huyo.
Mpira uliopigwa na Wayne Rooney ukiwa umempita tobo kipa wa Manchester City na kuandika goli
Raheem Sterling akiachia shuti na kuisawazishia Manchester City goli na kufanya matokeo kuwa 1-1
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni